Jumanne, 3 Novemba 2015

MAZINGIRA HAYA SI SALAMA KWETU

Unapoingia barabarani kuandamana kupinga unachopinga, Viongozi Wakuu wa Chama si sehemu ya Waandamaji. Hawa huandaa na kuhamasisha maandamano kwa nguvu kubwa ya kupinga MAZUIO yote ya Serikali na kutengeneza MGOGORO kati ya Waandamanaji na vyombo vya DOLA ya kufurumishana na kulipuliwa mabomu. Viongozi wanakuwa wametangulia kwenye viwanja vya mikutano na hotuba zao MIKOBANI kusubiri kupokea na kuhutubia WAANDAMAJI tu. Mazingira haya ni kutolewa KAFARA na Wanasiasa kwa maslahi binafsi ya WANASIASA. JITENGE NA MATAMKO YA USHIKINIZI YA WANASIASA, si salama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni